Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Shamra Shamra za CCM Zatikisa Boma Ng’ombe, Wananchi Wajaa Uwanjani

  • 3
Scroll Down To Discover

Wananchi wa Boma Ng’ombe, wilayani Hai mkoani Kilimanjaro, wamejitokeza kwa wingi kushiriki katika mkutano wa hadhara wa Kampeni za Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika tarehe 01 Oktoba, 2025.

Mkutano huo ulivuta hisia kubwa za wananchi waliokusanyika kusikiliza sera na mikakati ya chama hicho kuelekea uchaguzi. Shamra shamra, nyimbo na nderemo vilitawala uwanjani huku wafuasi wa CCM wakionesha mshikamano na kuunga mkono wagombea wao.

Viongozi wa chama hicho walitumia nafasi hiyo kueleza mafanikio yaliyopatikana na kuahidi kuendelea kusimamia maendeleo ya wananchi ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma za kijamii, miundombinu na uchumi wa wananchi wa Hai na mkoa wa Kilimanjaro kwa ujumla.



Prev Post Dar Es Salaam: Mkuu Wa Mkoa Chalamila Ahaidi Kuondoa Shida Ya Mwendokasi Kimara
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook