Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Mkurugenzi wa FBI Awataka Watu Kutoombeleza Kifo cha Mama Mlezi wa Tupac

  • 14
Scroll Down To Discover

Mkurugenzi wa FBI, Kash Patel

Mkurugenzi wa FBI, Kash Patel, ametoa kauli tata akiwataka watu kutoombeleza kifo cha Assata Shakur, mama mlezi wa Tupac

Assata Shakur, ambaye pia alijulikana kama Joanne Chesimard, aliefariki Alhamisi, Septemba 25, 2025, akiwa na miaka 78 mjini Havana, Cuba. 

Kifo chake kinasemekana kuwa ni kutokana na matatizo ya kiafya na umri mkubwa.

Patel alimtaja Assata kama gaidi, akiwakumbusha watu hukumu yake kwa kifo cha Afisa wa Polisi wa Jimbo la New Jersey, Werner Foerster, mwaka 1977. 

Alihukumiwa kwa mauaji ya daraja la kwanza mwaka huo huo, kisha alikimbia gerezani mwaka 1979 na kupata hifadhi Cuba, ambako aliishi hadi kifo chake mwaka 2025.

Assata Shakur, ambaye pia alijulikana kama Joanne Chesimard

Patel alisema: “Kumuombeleza ni kumsaliti afisi na damu ya kila polisi aliyetoa maisha yake kwa huduma.”

Kauli hii imeibua mjadala mkali, kwani baadhi ya watu wanamuona Assata kama shujaa wa kisiasa, huku wengine wakiiona kama hatari. Tukio hili linaonyesha historia changamano ya uhusiano kati ya polisi, haki za kiraia, na harakati za kisiasa nchini Marekani.



Prev Post FIFA Yaiadhibu Afrika Kusini kwa Kumchezesha Mchezaji Asiye na Sifa
Next Post BENKI YA EXIM IKISHIRIKIANA NA MATTERS YAUNGA MKONO MAFANIKIO YA WANAWAKE 
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook