Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

MATESO YA GAMONDI YANAMTESA PEDRO KWA YANGA

KOCHA mkuu wa Yanga, Pedro Gonçalves, amesema bado anabeba mzigo mkubwa wa kuhakikisha kikosi chake kinarejea katika ubora wa juu, licha ya matokeo mazuri ambayo wamekuwa wakiyapata kwenye michezo ya hivi karibuni. Pedro anasema anahisi deni kubwa la kulijenga upya jina la Yanga, ili iwe bora kuliko ilivyokuwa msimu uliopita. Msimu wa 2025 ulikuwa na misukosuko ndani ya benchi la ufundi la Yanga baada ya kuondoka kwa kocha Miguel Gamondi, ambaye alikuwa ametengeneza kikosi imara kilichoonesha kiwango cha juu. Baada ya Gamondi kuondoka, timu ilipitishwa kwa makocha wawili, akiwemo Saed Ramović na baadaye Hamdi Miloud aliyemaliza msimu kabla ya nafasi hiyo kumfikia Romain Folz. Hata hivyo, Folz hakudumu na hatimaye timu ikakabidhiwa kwa Pedro. Pedro anasema kupitia rekodi na ubora wa Yanga ya msimu uliopita, anajiona kwenye mtihani mkubwa na anairudisha timu hiyo kwenye kiwango kile kile au hata kuifikisha juu zaidi. “Mafanikio ya zamani yanaweka shinikizo, lakini pia yanaipa hamasa ya kuongeza ubunifu na mbinu mpya ndani ya kikosi. Ubora wa Yanga ya msimu uliopita unanipa picha ya kile kinachotakiwa kufikiwa, kazi yangu si tu kushinda mechi, bali kuijenga timu yenye utambulisho thabiti na uwezo mkubwa wa ushindani, msimu uliopita ulikuwa na viwango vinavyohitaji kufikiwa upya kwa jitihada za ziada,” amesema. Pedro ameongeza kuwa licha ya timu kutofanya vizuri kimataifa, bado walionesha upinzani mkubwa na kuendelea kutetea mataji yao ya ndani, likiwemo taji la Ligi Kuu Tanzania Bara. Hali hiyo inaonyesha kuwa msingi wa timu bado upo imara na unahitaji kupangwa upya kwa umakini. Kuhusu mabadiliko ya kikosi katika kila mchezo, Pedro amefafanua kuwa hajafanya hivyo kwa bahati mbaya, bali kwa ajili ya kupumzisha wachezaji waliocheza dakika nyingi msimu mzima. Ameeleza kuwa ni muhimu kuwasawazisha wote kwa kuwapa nafasi wale ambao hawajapata muda wa kutosha ili kuongeza ushindani ndani ya timu. Ameongeza kuwa wachezaji waliokuwa majeruhi sasa wanaanza kurejea taratibu, wanahitaji kupewa dakika chache katika michezo ili kurudisha utimamu wa miili yao. Lengo ni kuhakikisha kila mchezaji anakuwa fiti kwa ajili ya mechi zijazo. Akizungumzia ugumu wa kupata ushindi katika mchezo dhidi ya Coastal Union, Pedro amesema hali ya uwanja ilikuwa changamoto kubwa kwao, Amesisitiza kuwa “…inawezekana wenyeji wameuzoea.” Hata hivyo, ameahidi kuendelea kupambana ili kuhakikisha Yanga inapata matokeo bora bila kujali mazingira. The post MATESO YA GAMONDI YANAMTESA PEDRO KWA YANGA appeared first on Soka La Bongo.

Watanzania wafurika kununua bidhaa muhimu kwa hofu ya maandamano, katika Dira ya Dunia TV

Serikali ya Tanzania imewataka wananchi kusalia majumbani mnamo kesho Desemba 9, siku ambayo huadhimishwa kila mwaka kama Siku ya Uhuru wa Tanganyika. Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba, kufuatia kuibuka kwa taarifa za wito wa maandamano unaosambaa kupitia mitandao ya kijamii, hatua iliyoifanya serikali kuongeza tahadhari kuelekea siku hiyo muhimu ya kitaifa. Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw

ANAJIKUTA KWENYE SOKO LA USIKU LINALOMGHARIMU MAISHA YAKE UTAJIFUNZA KITU

🎬 Movie Title: NIGHT MARKET 🎞️ Genre: DRAMA, THRILLER 📺 Watch Full Movie Here: https://youtu.be/75uUPaasmJ8?si=n-7BN-RLty54s31S Credits: PAPAYAEX TVV Subscribe Her Channel: https://youtube.com/@papayaextvv?si=zAy25p-DxnCkDb90 _____________________________________ At E7Bits, we do short recaps to help Swahili-speaking audiences enjoy and understand African movies better. We DON’T own the movies — we promote them with respect. 📩 For takedown or promo requests, contact us via: e7bitscrew@gmail.com Hit Us Up: +255624944364 ______________________________________ Background Music Credits Alex Productions - ‘Elite’ is under a Creative Commons (BY 3.0) license: https://creativecommons.org/licenses/by/3.0/    / @alexproductionsnocopyright Music powered by BreakingCopyright: https://youtu.be/0Q7QpKVUlc8?si=GqQ9Znoueq-LVZxG #zeelakutune #zeelatown #e7bits #izkonka

Nafasi 293 za Ajira Serikalini

https://portal.ajira.go.tz/vacancies The post Nafasi 293 za Ajira Serikalini appeared first on SwahiliTimes.

The Wrecker (2025)

The road ends here. A car mechanic’s life takes an unexpected turn when his reckless brother makes a bad decision gaining the unwanted attention of a notorious crime boss. The Wrecker (2025) Genre: Action, Thriller Release Date: 2025 Stars: Tyrese Gibson, Harvey Keitel, Niko Foster, Mena Suvari, Chad Michael Collins Language: English Runtime: 95 mins

WADAU MADALE WAHIMIZWA KUJIUNGA NA SACCOS KWA USTAWI WA KIUCHUMI

Na John Bukuku – Dar es Salaam Mwenyekiti wa Madale Wadau Group, Bw. Stephen Kazimoto, ametoa ripoti maalum ikionyesha faida na umuhimu wa wanakikundi kujiunga na SACCOS kama njia ya kujenga uthabiti wa kifedha na kuongeza nguvu ya maendeleo ya kiuchumi kwa pamoja. Amesema SACCOS ni chombo muhimu cha kuweka akiba na upatikanaji wa mikopo yenye riba nafuu, hivyo wanachama wana nafasi kubwa ya kupanua biashara, kukabiliana na dharura na kuwekeza kwenye shughuli za kijamii kama elimu na ujenzi. Katika ripoti yake, Kazimoto amefafanua kuwa kupitia SACCOS wanachama hujengewa utamaduni wa kuweka akiba mara kwa mara, jambo ambalo linawaongezea hisa, nguvu ya kukopa na nidhamu katika matumizi ya fedha. Ameongeza kuwa mfumo huu huwasaidia kutimiza malengo yao ya kifedha kwa urahisi zaidi. Aidha, ameeleza kuwa wanachama wa SACCOS hupata gawio (dividends) kila mwisho wa mwaka kulingana na kiwango cha hisa walizowekeza, kitendo kinachowatia moyo wengi kuongeza akiba zao na kushiriki kikamilifu katika shughuli za chama. Bw. Kazimoto pia amebainisha kuwa SACCOS nyingi hutumia mifumo ya bima ya mikopo, hatua ambayo inalinda mali na maslahi ya wanachama, hivyo kupunguza hatari ya kupoteza fedha endapo changamoto zitajitokeza. Akizungumzia upande wa kujengewa uwezo, amesema wanachama hupata mafunzo ya ujasiriamali, uongozi, usimamizi wa fedha pamoja na mbinu za kilimo na biashara, jambo linaloongeza maarifa na uwezo wa kujitegemea kiuchumi. “Mara nyingi tunashuhudia faida ya ushirika kupitia msaada wa kifedha na kijamii pale mwanachama anapopatwa na changamoto. Ndio maana tunasisitiza kuwa nguvu ya pamoja ni msingi wa ustawi wetu,” amesema Kazimoto. Ripoti hiyo pia imeonyesha hali ya makusanyo ya kikundi ikiwa ni Shilingi 12,370,000/= zikiwemo Shilingi 2,750,000/= za kiingilio, Shilingi 5,100,000/= za hisa na Shilingi 4,529,000/= za ada. Akihitimisha, Mwenyekiti huyo amesema kujiunga na SACCOS ni hatua madhubuti kwa kikundi chochote kinacholenga kujijenga kiuchumi kwani kunatoa fursa ya mikopo nafuu, uwekezaji wa pamoja, usalama wa fedha na mtandao mpana wa ushirikiano. Amehimiza wanachama wa Madale Wadau Group kuendelea kujiunga ili kuongeza uwezo wa kufikia malengo ya pamoja na binafsi.


Deprecated: strip_tags(): Passing null to parameter #1 ($string) of type string is deprecated in /home/bongonet/domains/bongonet.co.tz/public_html/index.php on line 109

MANNAT 1-140|VASCO DJ

#mbosso #pawa # #photoshoot

Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.

MATESO YA GAMONDI YANAMTESA PEDRO KWA YANGA

Dege Mc Ft. Jeusi Mc & Buda Zoni – Ololo Remix

Daiva – Nishazama

Watanzania wafurika kununua bidhaa muhimu kwa hofu ya maandamano, katika Dira ya Dunia TV

ANAJIKUTA KWENYE SOKO LA USIKU LINALOMGHARIMU MAISHA YAKE UTAJIFUNZA KITU

Nafasi 293 za Ajira Serikalini

PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO DISEMBA 08, 2025

The Wrecker (2025)

WADAU MADALE WAHIMIZWA KUJIUNGA NA SACCOS KWA USTAWI WA KIUCHUMI

Nada Mreno – Zuchu

MANNAT 1-140|VASCO DJ

#mbosso #pawa # #photoshoot

Udi – Shobo sitaki

Loading views...
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook